Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Monday 1 July 2013

Rais Obama atilia mkazo amani mashariki mwa Kongo


Rais Barack Obama wa Marekani amezitaka nchi zinazopakana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuacha mara moja uungaji mkono wao kwa makundi ya waasi nchini humo.
Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari Ikulu mjini Dar es Salaam akiwa na mwenyeji wake Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, Rais Obama pia amemtaka Rais Joseph Kabila wa Kongo kupanga mikakati ya haraka ya kulikarabati na kulijenga upya jeshi la nchi hiyo. Rais wa Marekani ameongeza kuwa, wananchi wa Kongo wanahitaji kupewa fursa, kwani mapigano ya miaka kadhaa nchini humo yamewanyima fursa ya kupiga hatua za kimaendeleo.
Obama amesema kuwa, makubaliano ya amani yaliyotiwa saini mwezi Februari mwaka huu yenye lengo la kurejesha amani na utulivu mashariki mwa Kongo hayapaswi kubaki kwenye makaratasi bali yanabidi kufanyiwa kazi. Rais Barack Obama wa Marekani aliwasili Tanzania jana alasiri kwa ziara ya siku mbili, baada ya kuzitembelea nchi za Senegal na Afrika Kusini.

0 comments:

Post a Comment