Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday 11 May 2013

ALIYOYASEMA SHEKH PONDA SIKU MOJA BAADA YA KUTOKA JELA, NI PALE MSIKITI WA MTAMBANI KINONDONI JIJINI DAR ES SALAAM.



 
Umati mkubwa wa waumini walimiminika kutaka kusikia mawaidha yake kwa mara ya kwanza baada ya kutoka gerezani juzi. Katika tukio hilo, waumini pia walichanga fedha kwa ajili kumwezesha Sheikh Ponda kugharimia matibabu ya afya yake na sehemu ya fedha hizo walipewa mawakili wake ili wafanye maandalizi ya kukata rufaa.
Pia Mei 18 mwaka huu, waumini hao wamepanga kufanya dua (Itikafu) itakayofanyika katika msikiti wa mtambani kwa ajili ya kumwombea Sheikh Ponda na wenzake.

ust Mukadam alimshukuru Allah kwa kuwapa adhabu ya ugonjwa,watu kadhaa akiwemo 'mkubwa mmoja' alie mahu2ti sauz afrika(alihusika kuwatengenezea mashtaka),na afisa mwingne wa jesh kufarik ajalini baada ya kuwanyanyasa selo! Pia mkubwa mmoja wa jesh ambae ni msabato kuwatamkia kua 'waislamu mnaonewa' mara baada ya kuwahoji. Akamaliza kwa kusema 'ni wakati wa waislamu kujipanga' nae SHEIKH PONDA. alisema

'nitapambana hadi mwisho' huku watu wakisema takbir alah akbar! Amesema Wakristo wanapendelewa na serikali. Serikali ilisema aliekojolea kuran ni mtoto,wakati ye kawakuta watoto jela! Akiwemo wa miaka 10,aliyekwapua mkoba.,ila yule mkristo wa miaka 14 serikali ilisema mtoto na haikumchukulia hatua zozote!
“Wamekuwa wakinitungia njama za kuniondoa kwa misingi ya kuwa mimi siyo Mtanzania, hakuna wa kuniondoa hapa nchini na nitapambana hadi hatua ya mwisho na kuhakikisha kuwa Waislamu wanapata uhuru wao,” alinena Sheikh Ponda.

Pia kasema anazo cd,zikionyesha jins serikali inavoua na kupanga kukandamiza uislamu.pia Kampongeza sana Zitto kabwe kwa mchango wake wa kutetea uislamu bungeni na kamponda yule aliepeleka cd alizoita za uchochezi bungeni! Karudia kusisitiza kuwa NECTA kuna udini na Waislamu wanafelishwa! na pia serikali inapendelea na kuendeshwa na wakristo. Pia alihoji kuhusu bomu la Arusha kuwa, wamekamatwa waarabu ,mbona hawajakamata wazungu? Anasema huo ni mpango wa kuonea waarabu na uislamu!

Pia kasema wakristo hawajawahi kuuwawa na serikali,ila waislamu tu ndo wanauawa! Mwembechai waliuawa, Pemba waliuawa. na hata Pemba Waislamu waliuawa na serikali iki2mwa na Kanisa! amesema pemba kuna helcopter zilikua zinalipua majahazi ya waislamu(wakiwa baharini) wakati wanakimbilia Mombasa na Tanga.!
Pia kasema,nchi hii hakuna udini,ila kuna mapambano ya waislamu kudai haki zao na redio iman imefungiwa kuwaonea waislamu wasipate pa kusemea(ile ya wakristo haikua lengwa)!Kwa kifupi shekh kaapa atapambana kwa nguvu kubwa.

pia alihudhuria Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alielezea kusikitishwa kwake juu ya kauli kwamba Sheikh Ponda asingeweza kupata dhamana katika kesi iliyokuwa ikimkabili.

“Vyombo vyetu haviko makini, tuliambiwa Ponda hawezi kupata dhamana lakini leo hii amefungwa kifungo cha nje, hii inatia shaka na uamuzi uliokuwa ukiendelea,” alisema Profesa Lipumba.

0 comments:

Post a Comment