Serikali ya Uturuki imesema kuwa huenda ikaitisha kura ya maoni
kuhusiana na mpango wa kubomolewa bustani ya Gezi iliyoko karibu na
meidani ya Taksim mjini Istanbul ili kujaribu kumaliza maandamano ya
kupinga serikali yanayoendelea nchini humo.
Huseyin Celik, msemaji wa chama tawala cha AKP amesema hayo baada ya
mazungumzo yaliyofanyika kati ya Waziri Mkuu Recep Tayyip Erdogan na
baadhi ya wawakilishi wa wandamanaji mjini Anakara. Celik amesema, suala
hilo litaamuliwa kwa kura ya maoni ili uamuzi utakaochukuliwa umalize
maandamano na mikusanyiko kwenye bustani hiyo.
Hayo yanajiri huku waandamanaji wakiendelea kujikusanya kwenye meidani ya Taksim karibu na bustani ya Gezi na kuendelea kupambana na polisi wanaotumia nguvu kuwatawanya. Jeshi la polisi nchini Uturuki limetuhumiwa kutumia nguvu za ziada kuwatawanya waandamanaji.
Machafuko nchini Uturuki yalianza Mei 31 baada ya polisi kuwatawanya wandamanaji kwa maji na gesi za kutoa machozi wakati waandamanaji hao walipokuwa wanapinga kubolewa bustani hiyo ambayo ni eneo muhimu la makutano ya watu mjini Istanbul.
Hayo yanajiri huku waandamanaji wakiendelea kujikusanya kwenye meidani ya Taksim karibu na bustani ya Gezi na kuendelea kupambana na polisi wanaotumia nguvu kuwatawanya. Jeshi la polisi nchini Uturuki limetuhumiwa kutumia nguvu za ziada kuwatawanya waandamanaji.
Machafuko nchini Uturuki yalianza Mei 31 baada ya polisi kuwatawanya wandamanaji kwa maji na gesi za kutoa machozi wakati waandamanaji hao walipokuwa wanapinga kubolewa bustani hiyo ambayo ni eneo muhimu la makutano ya watu mjini Istanbul.
0 comments:
Post a Comment