Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imehairisha kesi ya mfanyabiashara Razah
Hussein Ladha na wenzake 10 wanaokabiliwa na jumla ya makosa 24 ya kuua
bila kukusudia kufuatia jengo la ghorofa 16 kubomoka jijini Dar es
Salaam na kuua watu 36.
Washitakiwa wengine ni Godluck Mbaga, Wilbroad Mugabisyo, Ibrahim Kisoki, Mohamed Abdubakari, Charles Salu, Zonazea Anage,Vedasto Ferand, Michael Hemed Hemed, Albert Jones na Joseph Ringo.
Kesi hiyo ilihairishwa jana na Hakimu Devotha Kisoka, kutokana na upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika, na itakuja tena Julai 15, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.
Awali walisomewa mashitaka 24 yanayowakabili ambayo yanafanana ya kuua bila kukusudia kinyume na kifungu cha 195 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, kuwa Machi 29 mwaka huu katika eneo la Mtaa wa Indira Gandhi waliwaua watu bila kukusudia.
Hata hivyo washitakiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo na kwamba mahakama yenye mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo ni Mahakama Kuu.
Machi 29 mwaka huu, ghorofa mmoja lililokuwa linajengwa katika mtaa wa Indira Gandhi lilianguka na kusababisha watu 36 kupoteza maisha.
Washitakiwa wengine ni Godluck Mbaga, Wilbroad Mugabisyo, Ibrahim Kisoki, Mohamed Abdubakari, Charles Salu, Zonazea Anage,Vedasto Ferand, Michael Hemed Hemed, Albert Jones na Joseph Ringo.
Kesi hiyo ilihairishwa jana na Hakimu Devotha Kisoka, kutokana na upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika, na itakuja tena Julai 15, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.
Awali walisomewa mashitaka 24 yanayowakabili ambayo yanafanana ya kuua bila kukusudia kinyume na kifungu cha 195 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, kuwa Machi 29 mwaka huu katika eneo la Mtaa wa Indira Gandhi waliwaua watu bila kukusudia.
Hata hivyo washitakiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo na kwamba mahakama yenye mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo ni Mahakama Kuu.
Machi 29 mwaka huu, ghorofa mmoja lililokuwa linajengwa katika mtaa wa Indira Gandhi lilianguka na kusababisha watu 36 kupoteza maisha.
0 comments:
Post a Comment