Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday 29 June 2013

Picha za Obama zateketezwa Afrika Kusini

                                 21 shaaban,1434 Hijiriyah/ 30 june,2013 Miyladiyah
Polisi nchini Afrika Kusini leo wamepambana na waandamanaji waliokuwa na hasira ambao wameteketeza moto picha za Rais Barack Obama wa Marekani ambaye yuko safarini nchini humo.
Waandamanaji hapo pia wameteketeza moto bendera za Marekani katika maandamano yaliyofanyika nje ya Chuo Kikuu cha Johannesburg, tawi la Soweto, sehemu ambayo Obama aliwahutubia wanafunzi.
Waandamanaji wamelaani vikali uungaji mkono wa Marekani kwa utawala haramu wa Israel na vile vile sera za Washington za kutumia ndege zisizo na rubani ambazo zimesababisha vifo vya watu wengi wasio na hatia hasa wanawake na watoto. Aidha wamemkosoa vikali Obama kwa kutotekeleza ahadi yake ya kufunga jela ya kuogofya ya Guantanamo inayosimamiwa na jeshi la Marekani. Wanaharakati walikuwa wamebeba mabango yaliyo kuwa na maandishi kama vile 'Obama acha kuunga mkono utawala wa ubaguzi wa rangi Israel'. Wanaharakati hao wanasema ni unafiki mkubwa kwa Obama kujaribu kujikurubisha kwa Shujaa Nelson Mandela aliyepinga utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini na wakati huo huo Washington inaendelea kuupa himaya kamili utawala haramu wa Israel unaowabagua Wapalestina.

0 comments:

Post a Comment