Mzingiro wa utawala wa Kizayuni wa Israel
dhidi ya Ghaza unaingia mwaka wake wa sita katika mwezi huu wa Juni ambapo
maelfu ya Wapalestina wanaendelea kukumbwa na masaibu ikiwa ni pamoja na kukosa
haki za msingi za binaadamu.
Gaza imekuwa chini ya mzingiro wa utawala
haramu wa Israel kutoka mwezi Juni mwaka 2007. Mzingiro huo wa kinyama
umepelekea hali ya maisha kuzorota kwa sababu Israel imewazuia wakaazi wa Ghaza
haki ya kununua vyakula, dawa na vifaa vya ujenzi. Jo Harisson wa shirika la
kutoa misaada ya Okfam anasema asilimia 80 ya Wapalestina huko Ghaza wanaishi
kwa kutegemea misaada. Mtetezi wa haki za binaadmau kutoka Uingereza Adie
Mormech anasema jamii ya kimataifa haijachukua hatua zozote kusitisha mzingiro
wa Israel dhidi ya Wapalestina huko Ghaza. Anasema Ghaza ina idadi ya watu
milioni 1.7 ambapo nusu yao ni watoto. Mtetezi huyo wa haki za binaadmau
anasema kuwaadhibu watu wa Ghaza ni jambo ambalo linakiuka sheria za kimataifa.
Israel iliweka mzingiro wa ardhi, anga na baharini dhidi ya watu wa Ghaza baada
ya hatua yao ya kuichagua serikali ya Harakati ya Kiislamu ya Palestina Hamas
katika uchaguzi wa kidemokrasia
0 comments:
Post a Comment