Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Tuesday 18 June 2013

MABOMU YA MACHOZI YARINDIMA Arusha

                       
RPC Arusha, Liberaus Sabas
Hali si shwari katika uwanja wa Soweto  Arusha kufuatia mabomu ya machozi kupigwa ili kutawanya watu waliokusanyika katika viwanja hivyo kwa ajili ya kuuga miili ya marehemu waliokufa kwenye mlipuko wa bomu hivi juzi.
Habari kutoka mitandao mbalimbali zinaeleza kuwa wabunge wa CHADEMA wametanyika kila mmoja upande wake na kadhaa inadaiwa kuwa wamekamatwa na polisi. Mabomu ya machozi yanapigwa maeneo mbalimbali ya jiji hilo na watu wamejifungia majumbani mwao.
Awali Jeshi la polisi lilipiga marufuku CHADEMA kufanya shughuli zozote za kuaga miili ya marehemu kwenye viwanja vya Soweto kwani zoezi la uchunguzi bado linaendelea kwenye viwanja hivyo huku mabomu yakirindima uwanjani hapo.
Akizungumza ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani hapa Liberatus Sabas alisema kutokana na uchunguzi unaoendelea wa tukio la bomu kwenye viwanja hivyo imeonelea kuwa si busara kuweka mkusanyiko wa watu kwani kutaharibu upelelezi.
Kamanda Sabas alisema kuwa kwa hiyo jeshi hilo limewataka viongozi wa chama hicho kuwaeleza wafuasi wao mahali sahihi watakapoweza kufanyia shughuli hiyo lakini si kwenye viwanja hivyo.
Hali kwenye viwanja hivyo imekuwa ya pilika pilika tangia juzi kwa wafuasi wa chama hicho kujikusanya tokea asubuhi hadi jioni kwa madai ya kuomboleza tukio la bomu la kurushwa kwa mkono lililotokea uwanjani hapo juzi.
Hata hivyo viongozi wa chama cha demokrasia na maendeleo walikuwa wamukusanyana kwenye uwanja huo hali iliyoendelea kuleta mvutano kati ya viongozi  wa jeshi la polisi na  wafuasi hao baada ya kukaidi amri ya jeshi hilo mabomu yalirindima uwanjani hapo.
Baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho walikuwepo uwanjani hapo akiwemo mbunge wa jimbo la ubungo John Mnyika,Ezekia Wenje na wabunge mbali mbali wa chama hicho walikuwa kwenye kikao cha bunge kinachoendelea hali hiyo imeliweka jiji hili kusimama shughuli zake kutokana na mabomu hayo. Chanzo: Fuullshangweblog na mitandao mingine.

 

0 comments:

Post a Comment