21Rajab,1434
Hijiriyah/ May 31,2013 Miyladiyah
Duru za habari nchini Sudan zinaarifu kuwa, mapigano ya kikabila
yaliyotokea katika jimbo la Darfur Kusini yamepelekea watu wasiopungua
64 kuuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa. Gazeti la Al-Ahram
linalochapishwa nchini Sudan limewanukuu viongozi wa jimbo la Darfur
Kusini wakithibitisha kujiri mapigano makali kati ya makabila mawili
katika jimbo hilo yaliyosababisha wa 64 kuuawa. Kwa mujibu wa ripoti
hiyo, mwezi Machi mwaka huu, kulitokea pia mapigano makali kati ya
makabila hayo mawili huku chanzo kikitajwa kuwa ni tofauti kuhusiana na
ardhi. Migogoro ya kikabila imeshtadi katika siku za hivi karibuni
katika jimbo la Darfur. Siku kadhaa zilizopita pia, watu 130
waliuawa baada ya kutokea mapigano ya kikabila huko magharibi mwa jimbo
hilo nchini Sudan.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment