21Rajab,1434
Hijiriyah/ May 31,2013 Miyladiyah
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema Tume ya Mishahara na Marupurupu
SRC ndiyo iliyopewa jukumu la kikatiba la kuamua mishahara ya maafisa
wote wa serikali na kulitaka Bunge liheshimu maamuzi ya tume hiyo.
Kiongozi huyo ametoa wito kwa wabunge kushauriana na SRC na kutatua
mzozo kuhusu mishahara yao. Rais Kenyatta amesema maafisa wote wa umma
na serikali kuu wataendelea kuheshimu mishahara ya SRC. Rais wa Kenya
amesema kupitia taarifa kwamba amekasirishwa mno na malumbano ambayo
yamekuwa yakiendelea kwa majuma kadhaa kati ya wabunge na tume ya SRC.
Taarifa yake inafuatia hatua iliyochukuliwa na wabunge siku ya Jumanne
ya kufuta ilani ya SRC iliyopunguza mishahara ya wabunge kutoka shilingi
851, 000 hadi 532, 000. Mwenyekiti wa SRC, Bi. Sarah Serem amesema
chombo chochote kitakachoongeza mishahara ya wabunge kitachukuliwa hatua
za kisheria kwani tume yake ndiyo yenye mamlaka ya kikatiba ya kuongeza
au kupunguza mishahara ya watumishi wa umma na maafisa wa serikali.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment