21Rajab,1434
Hijiriyah/ May 31,2013 Miyladiyah
Waziri wa Mambo ya Ndani anayeondoka nchini Uganda, Hillary Onek ametoa
amri kwa polisi kuondoka mara moja kwenye makao makuu ya shirika la
Monitor Publications linalochapisha gazeti la kila siku la Daily
Monitor. Onek amesema shirika hilo liko huru kuendesha shughuli zake
bila ya kubughudhiwa na yeyote. Duru za habari zinaarifu kuwa, polisi
tayari wameondoka kwenye shirika hilo na wafanyakazi wameanza shughuli
zao. Itakumbukwa kuwa, polisi walivamia makao makuu ya shirika hilo Mei
20 na kulizingira hadi mapema leo asubuhi kwa madai kwamba gazeti la
shirika hilo lilichapisha habari yenye kuhatarisha usalama wa taifa.
Kitendo cha polisi kuvamia Monitor Publicationsh kililaaniwa na
mashirika mbalimbali ya kimataifa ukiwemo Umoja wa Mataifa.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment