Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 30 May 2013

Mtuhumiwa mauaji ya kimbari Rwanda akamatwa

                                21Rajab,1434 Hijiriyah/ May 31,2013 Miyladiyah
 Mtuhumiwa wa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 nchini Rwanda, ametiwa mbaroni nchini Norway. Habari kutoka Norway zinasema kuwa, mtu huyo aliyetiwa mbaroni anatuhumiwa kutenda jinai tofauti wakati wa mauaji ya kimbari na kwamba, alikuwa akiishi nchini humo kwa kipindi cha miaka 13. Leo mahakama ya nchi hiyo inatarajiwa kuchukua uamzi kuhusiana na kadhia hiyo. Wakili wa mtuhumiwa huyo Harald Stabell amesema kuwa, mteja wake hakuhusika kwa vyovyote na mauaji ya kimbari nchini Rwanda, yaliyopelekea watu laki nane kuuawa sambamba na kutaka aachiliwe huru. Televisheni moja nchini Norway imetangaza kuwa, mwaka uliopita mtuhumiwa huyo alitiwa mbaroni kwa tuhuma hizo na kuachiliwa huru hapo baadaye. Mauaji ya kimbari nchini Rwanda, yalitokea mwaka 1994 baada ya kuanguka ndege iliyokuwa imembeba rais wa wakati huo Juvenal Habyarimana karibu na mji mkuu wa nchi hiyo Kigali.

0 comments:

Post a Comment