Kiongozi wa Harakati ya Ukombozi ya Wananchi wa Sudan ametangaza kuwa,
hatua ya kuakhirishwa safari ya Rais Salva Kiir wa nchi hiyo huko Sudan,
haihusiani na tuhuma zilizotolewa na Khartoum kwa serikali ya Juba, juu
ya kuhusika kwake katika mashambulizi ya waasi ya hivi karibuni huko
magharibi mwa Sudan. Hayo yamesemwa na Atim Garang kiongozi wa ngazi za
juu wa Harakati ya Ukombozi ya Wananchi wa Sudan huko kusini mwa nchi
hiyo na kuongeza kuwa, uakhirishwaji wa safari hiyo ya kiongozi huyo,
hauna mafungamano yoyote na tuhuma hizo. Kiongozi huyo amesema kama
ninavyomnukuu, "inaonekana viongozi wa Sudan wana wasiwasi na mabadiliko
ya Darfur na Kordofan, hivyo wanapanga mkutano wa Rais Salva Kiir wa
Sudan Kusini na Omar Hassan Al-Bashir wa Sudan, ufanyike kando ya
mkutano ujao wa Umoja wa Afrika, utakaofanyika mjini Addis Ababa
Ethiopia." Mwisho wa kunukuu. Wiki iliyopita, balozi wa Sudan Kusini
mjini Khartoum Myan Dott, alinukuliwa akisema kuwa, safari ya Rais Salva
Kiir wa Sudan Kusini nchini Sudan iliyokuwa imepangwa kufanyika mwezi
huu, imesogezwa mbele hadi katikati ya mwezi ujao wa Juni.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment