Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Monday 20 May 2013

Walioushambulia msafara wa waziri wanaswa Misri

 
Duru za habari zimemnukuu afisa mmoja wa usalama nchini Misri akisema kuwa, watu wanne wametiwa mbaroni kwa tuhuma ya kushambulia msafara wa Waziri wa Mambo ya Ndani wa nchi hiyo. Afisa huyo ambaye ni kiongozi wa idara ya usalama mjini Cairo amewambia waandishi wa habari kuwa, idadi ya watu waliotiwa mbaroni kwa kuhusika katika shambulizi hilo lililotokea katika mji wa Nasr dhidi ya msafara wa Muhammad Ibrahim, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Misri,  imefikia wanne. Shambulizi hilo lilitokea katika mtaa wa Mustapha al-Nuhas mjini Nasr, baada ya kuzuka mapigano katika mtaa huo kati ya watu wenye silaha waliokuwa wakigombania umiliki wa eneo mjini hapo. Aidha wakati mapigano hayo yakiendelea, msafara wa waziri huyo wa mambo ya ndani wa Misri na ambaye anaishi katika mji huo, ulikuwa ukipita na hivyo kushambuliwa. Wiki kadhaa zilizopita pia, Waziri Mkuu wa nchi hiyo Hisham Qandil, alinusurika kifo baada ya mtu mmoja mwenye silaha kuushambulia msafara wake katika viunga vya mji mkuu Cairo.

0 comments:

Post a Comment