Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Monday 20 May 2013

Wafungwa wa Gitmo waungwa mkono Uingereza

 Wanaharakati nchini Uingereza, wamefanya maandamano mjini London, wakiwaunga mkono wafungwa wa jela ya Guantanamo. Maandamano ya wanaharakati hao waliokuwa wamevalia mavazi yanayofanana na yale ya wafungwa wa jela ya Guantanamo, yalifanyika mbele ya ubalozi wa Marekani mjini London na kuonyesha mafungamano wao na wafungwa wa jela hiyo. Hii ni katika hali ambayo, siku ya Ijumaa iliyopita, kundi moja la wanaharakati wa Marekani waliovalia mavazi kama hayo walikusanyika mbele ya ikulu ya Marekani White House na kutaka kuachiliwa haraka wafungwa hao. Karibu wafungwa 130 wa jela hiyo ya kutisha wanaendelea na mgomo wao wa kula chakula kwa siku 103 sasa, wakilalamikia hali mbaya ya jela hiyo. Ni vyema kuashiria hapa kuwa, baada ya Rais Barack Obama wa Marekani kuingia madarakani, aliahidi kuifunga jela hiyo, lakini hajatekeleza ahadi hiyo.

0 comments:

Post a Comment