Makosa mengi yamekuwa yakifanyika wakati wa kufanyika oparesheni kwenye
hospitali kadhaa za serikali nchini Uingereza. Taarifa iliyotolewa na
Taasisi ya Kitaifa ya Afya na Tiba ya Uingereza imeeleza kuwa, katika
kipindi cha miaka minne iliyopita, jumla ya makosa makubwa 762
yalifanywa wakati wa kufanyika upasuaji katika hospitali za serikali
nchini humo. Dakta Michael Durkin Afisa wa Usalama wa Wagonjwa katika
taasisi hiyo amekiri juu ya kutokea makosa hayo na kusema kuwa,
kupatikana makosa zaidi ya 700 katika kipindi cha miaka minne, ni janga
kubwa kwa taifa hilo.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment