Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Friday 10 May 2013

Dikteta wa Guatemala afungwa miaka 80 jela



Efrain Rios Montt Rais wa zamani wa Guatemala amehukumiwa adhabu ya kifungo cha miaka 80 jela, baada ya kupatikana na hatia ya kutenda jinai za kivita nchini humo. Mahakama Kuu ya Guatemala jana ilimhukumu dikteta Montt adhabu hiyo baada ya kumpata na hatia ya kufanya mauaji ya kizazi, jinai za kivita, ubakaji na mauaji ya halaiki dhidi ya wananchi wa kabila la Maya nchini humo. Taarifa zinasema kuwa, Jenerali Efrain Montt mwenye umri wa miaka 86, alifanya mauaji ya halaiki dhidi ya watu wa kabila hilo wakati alipoongoza mapinduzi ya kijeshi mwaka 1982 nchini humo. Imeelezwa kuwa, zaidi ya watu 1,700, waliuawa kwenye machafuko hayo yaliyotokea nchini humo.

0 comments:

Post a Comment