Vyombo vya habari vya Bangladesh vimeripoti kuwa, mwanamke mmoja
aliyekuwa anafanya kazi kwenye kiwanda cha ushonaji wa nguo nchini humo,
ameopolewa kwenye kifusi cha ghorofa akiwa hai baada ya kupita siku 17
tokea litokee tukio hilo. Taarifa zinasema kuwa, mwanamke huyo
ameopolewa akiwa chini ya kifusi, wakati zoezi la kufukua na kuondoa
viwiliwili bado linaendelea nchini humo. Hadi sasa zaidi ya wahanga
elfu moja wameshaondolewa chini ya kifusi kwenye jengo hilo lililokuwa
na ghorofa nane. Inafaa kuashiria hapa kuwa, jengo la ghorofa nane
lililokuwa likitumiwa na kiwanda cha ushonaji wa nguo liliporomoka siku
ya tarehe Jumanne ya tarehe 23 Aprili mwaka huu.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment