Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday 11 May 2013

Kenyatta ataka mashirikiano zaidi kwa nchi za Kiafrika



Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ametaka yawepo mashirikiano zaidi kwa nchi za Kiafrika. Akizungumza mwishoni mwa kikao cha Jukwaa la Kimataifa la Uchumi mjini Cape Town nchini Afrika Kusini hapo jana, Rais Uhuru Kenyatta ameongeza kuwa, mashirikiano ya kieneo na uthabiti wa amani, ni miongoni mwa malengo ya kimsingi ya nchi za Kiafrika yenye shabaha ya kuelekea kwenye ustawi katika miongo ijayo. Aidha ametaka zifanyike juhudi za kuwepo soko moja lenye nguvu katika eneo la ukanda wa Afrika Mashariki. Inafaa kuashiria hapa kuwa, lengo la kufanyika kikao kama hicho cha kimataifa, ni kuchunguza changamoto za kiuchumi na kijamii zinazolikabili bara la Afrika na hali kadhalika kupanga mikakati mipya yenye shabaha ya kuinua na kuiboresha zaidi sekta ya uchumi katika nchi za Kiafrika.

0 comments:

Post a Comment