Rais Hassan Sheikh Mohamoud wa Somalia ametoa wito wa uwekezaji
zaidi katika nchi yake ambayo inajikwamua kutoka katika machafuko ya
zaidi ya miongo miwili. Ameswema hayo leo Jumanne katika ufunguzi wa
Kongamano la Kimataifa kuhusu Somalia linalofanyika London, Uingereza.
Wawakilishi wa zaidi ya nchi 50 pamoja na taasisi za kimataifa
wameshiriki katika kongamano hilo la siku moja ambalo linalenga kusaidia
ujenzi mpya wa Somalia baada ya mgogoro wa muda mrefu. Rais Mohamoud
amesema kuwa, kadhia ya Somalia ni muhimu kwani ina taathira kieneo na
dunia nzima.
Kongamano hilo la wafadhili wa Somalia pia limehudhuriwa na viongozi wa nchi zinazopakana na Somalia akiwemo Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya.
Aidha wawakilishi wa Shirika la Fedha Duniani, Benki ya Dunia, Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa nao wamehudhuria mkutano huo.
Wakati huo huo imearifiwa kuwa mkuu wa Shirika la Kijasusi la Qatar ameuawa katika mripuko wa bomu mjini Mogadishu jana Jumatatu. Kwa mujibu wa gazeti la Ad-Diyar la Lebanon, jasusi huyo mkuu wa Qatar alikuweko Somalia kupanga namna magaidi kutoka Yemen watakavyotumwa Syria baada ya kupewa mafunzo na vikosi maalumu vya Marekani nchini Qatar.
Kongamano hilo la wafadhili wa Somalia pia limehudhuriwa na viongozi wa nchi zinazopakana na Somalia akiwemo Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya.
Aidha wawakilishi wa Shirika la Fedha Duniani, Benki ya Dunia, Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa nao wamehudhuria mkutano huo.
Wakati huo huo imearifiwa kuwa mkuu wa Shirika la Kijasusi la Qatar ameuawa katika mripuko wa bomu mjini Mogadishu jana Jumatatu. Kwa mujibu wa gazeti la Ad-Diyar la Lebanon, jasusi huyo mkuu wa Qatar alikuweko Somalia kupanga namna magaidi kutoka Yemen watakavyotumwa Syria baada ya kupewa mafunzo na vikosi maalumu vya Marekani nchini Qatar.
0 comments:
Post a Comment