Maelfu ya wafanyakazi wa Umoja wa Ulaya, wameendelea na mgomo katika
kulalamikia utekelezaji wa mpango wa kubana matumizi katika nchi za
jumuiya hiyo. Leo wafanyakazi 3500 wa Baraza la Umoja wa Ulaya wamefanya
maandamano mgomo mjini Brussels, Ubeligiji, kulalamikia kupunguzwa
mishahara ya wafanyakazi na kuongezwa masaa ya kazi katika nchi za umoja
huo. Navyo vyama vya wafanyakazi barani Ulaya vimetangaza kuwa, katika
kipindi cha miaka 15 iliyopita, wafanyakazi wa moja huo unaoundwa na
nchi wanachama 27, wamepungukiwa na asilimia 60 ya uwezo wa manunuzi,
suala ambalo linatokana na siasa za kubana matumizi za serikali za nchi
za bara hilo. Kuongezwa miaka ya kustaafu, ni miongoni mwa mambo
yananolalamikiwa pia na wafanyakazi wa nchi za Ulaya.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment