Mkuu wa Kamisheni Kuu ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa
Mataifa ameonya juu ya athari za uharibifu kwenye operesheni za vikosi
vya Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Akilihutubia Baraza la Usalama la umoja huo, Mary Robinson amesema kuwa,
vikosi vya kimataifa vilivyoko nchini Kongo vinapaswa kufanya
operesheni zake kwa uangalifu mkubwa ili kuepusha kujitokeza athari
mbaya na maafa nchini humo. Amesisitiza kuwa, iwapo operesheni hizo
hazitafanyika kwa njia sahihi, kuna hatari ya kujitokeza maafa makubwa
kwa wananchi wa nchi hiyo.
Inafaa kuashiria hapa kuwa, tarehe 29 Machi 2013 Baraza la Usalama liliafiki kutumwa vikosi vya kimataifa nchini Kongo kwa shabaha ya kukabiliana na makundi ya waasi.
Inafaa kuashiria hapa kuwa, tarehe 29 Machi 2013 Baraza la Usalama liliafiki kutumwa vikosi vya kimataifa nchini Kongo kwa shabaha ya kukabiliana na makundi ya waasi.
0 comments:
Post a Comment