Rais Faure Gnassingbé wa Togo amezikosoa vikali nchi za Magharibi
kwa kukata misaada yao kwa nchi hiyo na kusisitiza kwamba hatua hiyo
itazidisha vitendo vya kigaidi nchini humo.
Akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kinachojadili ugaidi barani Afrika, Rais Gnassingbé ameongeza kuwa, nchi za Magharibi zilichukua hatua za kidhulma kwa kukata misaada yao kwa serikali ya Lome mwaka 2008. Ameongeza kuwa, nchi za Magharibi zinapasa kutekeleza ahadi zao ilizozitoa kwa nchi zinazoendelea na hasa za Kiafrika, ili uchumi wa nchi hiyo ya Magharibi mwa Afrika ukue na kufikia kiwango cha asilimia 7 mwaka 2015.
Akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kinachojadili ugaidi barani Afrika, Rais Gnassingbé ameongeza kuwa, nchi za Magharibi zilichukua hatua za kidhulma kwa kukata misaada yao kwa serikali ya Lome mwaka 2008. Ameongeza kuwa, nchi za Magharibi zinapasa kutekeleza ahadi zao ilizozitoa kwa nchi zinazoendelea na hasa za Kiafrika, ili uchumi wa nchi hiyo ya Magharibi mwa Afrika ukue na kufikia kiwango cha asilimia 7 mwaka 2015.
0 comments:
Post a Comment