Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Tuesday 14 May 2013

Mpinzani wa Wazayuni akumbukwa Tunisia

                             


Wasomi na shakhsia mbalimbali wa kisiasa na kidiplomasia wa kieneo na kimataifa, wamefanya sherehe ya kumuenzi mwandishi na mwanamapambano mkubwa wa Tunisia aliyekuwa akipambana na utawala haramu wa Kizayuni Dkt. Hussein at-Triki. Sherehe hizo zimehudhuriwa na viongozi, wanasiasa na wanadiplomasia mbalimbali kutoka Iran, Lebanon, Algeria, Venezuela na nchi nyengine za dunia. Katika sherehe hizo Katibu Mkuu wa Chama cha al Ghad kinachounga mkono mapambano ya muqawama dhidi ya wavamizi wa Kizayuni nchini humo Omar al-Shahid, alizungumzia sifa ya kipekee aliyokuwa nayo Hussein at Turiki katika kupambana na dhuluma na kusema kwamba, msomi huyo alikuwa nguzo muhimu katika mapambano na Wazayuni. Mwezi Mei mwaka jana at Triki maarufu kwa jina la Sheikh wa wanamapambano wa Tunisia, aligongwa na gari wakati akitoka kusali katika msikiti uliokuwa karibu na nyumba yake na kufariki dunia akiwa hospitalini. Wakati huo huo kiongozi wa kundi la Kisalafi linalojulikana kwa jina la Ansaru al-Sharia, Seifu al-Din bin Huseein amesema kuwa, Tunisia inakaribia kuingia katika vita vya ndani. Seifu al-Din anayetafutwa na vyombo vya usalama vya nchi hiyo, ameitaja hatua ya serikali ya Tunis ya kuanzisha oparesheni dhidi ya ugaidi kuwa, ni kuanzisha vita vya ndani nchini humo.

0 comments:

Post a Comment