Mahakama ya jinai ya mjini Cairo, Misri imeakhirisha kusikiliza kesi ya
binamu yake Kanali Muammar Gaddafi wa Libya, Ahmed Gaddafi al Dam.
Habari zinasema kuwa, mahakama hiyo inayoongozwa na jaji Mustapha Hassan
Abdullah, imeamua kuakhirisha kusikiliza kesi ya al Dam, aliyekuwa
mratibu wa mahusiano kati ya Misri na Libya, kufuatia ombi la mawakili
wake waliotaka hukumu hiyo iakhirishwe hadi kesho tarehe 15 Mei. Mnamo
tarehe 9 mwezi Machi mwaka huu, askari wa usalama nchini Misri walifanya
operesheni yao katika eneo la Zamalek katikati ya mji mkuu Cairo
anakoishi binamu huyo wa Gaddafi, suala ambalo lilizusha mapigano kati
ya polisi wa Misri na walinzi wa Ahmed Gaddafi. Kufuati kitendo hicho,
Polisi ya Kimataifa Interpol ilitoa amri ya kutiwa mbaroni mtuhumiwa
huyo. Tarehe 19 mwezi huo huo Ahmed Gaddafi al Dam aliwafyatulia risasi
Polisi wa Kimataifa wa Interpol pamoja na polisi wa Misri katika wakati
walipojaribu kumtia mbaroni binamu huyo wa Kanali Muammar Gaddafi na
kumjeruhi afisa mmoja. Idara ya mahakama nchini Misri imepinga
kumkabidhi Ahmed Gaddaf al Dam kwa serikali ya Libya na imetangaza
kumshitaki katika mahakama zake huku ikiwa tayari imeshamsaili.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment