Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday 11 May 2013

Maelfu wakimbia machafuko Kordofan Kaskazini

                                   02,RAJAB,1434 Hijiriyah/ May 12,2013 Miyladiyah
Maelfu ya watu wameripotiwa kuyakimbia makazi yao katika jimbo la Kordofan Kaskazini huko Sudan kufuatia mashambulio ya hivi karibuni ya waasi katika jimbo hilo. 
Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kamati ya Misaada ya Kibinaadamu kwa wakimbizi wa Sudan. Suleiman Abdur- Rahman amesema kuwa, mashambulio ya waasi katika jimbo la Kordofan Kaskazini yamesababisha watu thelathini na mbili elfu kuwa wakimbizi. 
Taarifa zaidi zinasema kuwa, tayari serikali ya Sudan imeanzisha operesheni za upelekaji misaada na mahitaji ya lazima kwa wakimbizi hao walioyakimbia makazi yao baada ya kushadidi mashambulio ya waasi wanaojulikana kwa jina la Harakati ya Kimapinduzi. Wakati huo huo, 
Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, asasi za utoaji misaada zinazofungamana na umoja huo zimeanzisha operesheni za kupeleka misaada ya kibinaadamu katika baadhi ya maeneo ya Jimbo la Kordofan Kusini ambako nako hali ya kibinaadamu inaripotiwa kuwa mbaya.
 Martin Nersiky, Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, ofisi ya uratibu wa misaada ya kibinaadamu imesema kuwa, wafanyakazi wa ofisi hiyo wameshapatiwa suhula kwa ajili ya kuwahudumia watu elfu 40 ambao hivi karibuni waliyakimbia makazi yao katika jimbo hilo.

0 comments:

Post a Comment