Muungano wa Palestina Huru nchini
Afrika Kusini umeitaja Israel kuwa ni utawala wa Kibaguzi. Taarifa ya
muungano huo imelaani vikali muamala na hatua zisizo za kisheria na
zinazokinzana na ubinaadamu za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya
Wapalestina na kusisitiza kwamba, utawala huo hauna tofauti yoyote na
utawala wa zamani wa ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini. Muungano wa
Palestina Huru umesisitiza kwamba, hatua za kuyayahudisha maeneo ya
Wapalestina pamoja hatua za Israel za kuwapokonya Wapalestina haki zao
za kimsingi hazina maana nyingine ghairi ya ubaguzi.
Muungano huo umelaani pia hujuma na
jinai za kila leo za Israel dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina na
kusisitiza kwamba, Wazayuni hawatafanikiwa katika mipango yao ya
kuubadilisha mji mtakatifu wa Quds na kuufanya kuwa ni wa Kiyahudi;
kwani mji huo mtakatifu ni mali ya Wapalestina. Muungano wa Palestina
Huru nchini Afrika Kusini umetahadharisha pia kuhusiana na njama za
Wazayuni dhidi ya msikiti mtakatifu wa al-Aqswa.
0 comments:
Post a Comment