Kesi ya Hosni Mubarak, dikteta wa Misri
aliyeng’olewa madarakani pamoja na wanawe wawili wa kiume Alaa na Jamal,
waziri wa zamani wa Mambo ya Ndani wa utawala wake Habib El-Adly pamoja
na wasaidizi wake sita waandamizi imeanza kusikilizwa tena leo lakini
imeakhirishwa hadi tarehe 8 Juni.
Mubarak ambaye mwezi Juni mwaka jana
alihukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kushindwa kuwalinda raia wasio
na silaha katika vuguvugu la siku 18 la Mapinduzi ya wananchi
yaliyoung’oa madarakani utawala wake wa kidikteta mapema Februari mwaka
2011 alifunguliwa tena mashtaka mwezi Januari mwaka huu kutokana na
ukiukaji wa taratibu uliofanyika wakati aliposhtakiwa mara ya kwanza.
Itakumbukwa kuwa Jaji Mustafa Hassan Abdullah aliyesikiliza kwanza kesi
ya diktetka Mubarak na wenzake alijiondoa kusikiliza kesi hiyo mwezi
uliopita na kuihamishia kwenye mahakama ya rufaa. Kesi hiyo sasa
inasikilizwa na Jaji Mahmoud kamel El Rashidi ambaye ameaiahirisha hadi
tareh 8 Juni ili kutoa fursa kwa mahakama ya kupitia nyaraka za ushahidi
zenye kurasa 55,000…/
0 comments:
Post a Comment