Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday 11 May 2013

Muigai: Hatujataka kesi za ICC zisimamishwe

                                 02,RAJAB,1434 Hijiriyah/ May 12,2013 Miyladiyah
 Mwanasheria Mkuu wa Kenya amejiweka mbali na ombi la balozi na mwakilishi wa kudumu wa nchi hiyo katika Umoja wa Mataifa aliyelitaka Baraza la Usalama la umoja huo lisimamishe kesi zinazowakabili Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC.

Githu Muigai Mwanasheria Mkuu wa Kenya amenukuliwa leo akisema kuwa, serikali ya nchi hiyo haina taarifa na barua kama hiyo katika Umoja wa Mataifa na kwamba, huo sio msimamo rasmi wa serikali ya Nairobi.
 Githu Muigai ameongeza kuwa, msimamo rasmi wa serikali ya Kenya ni kushirikiana kikamilifu na Mahakama ya Kimataifa na kwamba, Nairobi ina lengo la kuendeleza ushirikiano huo
. Hayo yanajiri katika hali ambayo, wakili wa William Ruto juzi alitangaza kwamba, mteja wake hafanyi juhudi za kutaka kusitishwa kesi inayomkabili katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC.

Ikumbukwe kuwa, siku ya Alkhamisi Macharia Kamau Mwakilishi wa Kudumu wa Kenya katika Umoja wa Mataifa aliwasilisha barua katika Baraza la Usalama la umoja huo akitaka kusimamishwa kesi dhidi ya Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC.

0 comments:

Post a Comment