Msemaji wa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF), Gerry Rice amesema kuwa
uchumi wa Misri unaendelea kuporomoka na amedokeza kuwa Cairo haitopata
msaada wowote kutoka kwa shirika lake hadi pale itakapotoa ripoti mpya
kuhusu hali halisi ya kiuchumi. Mazungumzo ya IMF na Misri kuhusu mkopo
wa dola bilioni 4.8 yameshindwa kukamilika kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa
kutokana na kile kinachotajwa kuwa ni woga wa Cairo wa kuchukua maamuzi
magumu. Serikali ya Misri itatakiwa kupunguza matumizi, kuondoa ruzuku
katika bidhaa nyingi hususan mafuta na gesi pamoja na kupunguza idadi ya
wafanyakazi wa umma kabla ya kupokea mkopo huo. Weledi wa mambo
wanaamini kuwa. Cairo haiko tayari kuchukua hatua hizo kwa hofu kwamba
wananchi wataandamana na huenda wakaiangusha serikali ya Rais Mohammad
Mursi.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment