Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 9 May 2013

Bunge la Zimbabwe laidhinisha rasimu ya katiba mpya



Bunge la Zimbabwe hapo jana Alhamisi liliidhinisha rasimu ya katiba mpya baada ya mjadala mkali wa siku mbili. Wabunge 156 waliipigia kura ya ndio huku idadi ndogo ikiipinga rasimu hiyo ya katiba mpya. Kwa mujibu wa sheria za bunge, muswada wowote unahitaji thuluthi mbili au kura 140 kuweza kupita. Sasa rasimu hiyo iliyopitishwa kwa wingi wa kura kwenye kura ya maoni mwezi Machi,  itapelekwa kwenye bunge la Senet ambako inatarajiwa kupitishwa na kisha baadaye Rais Robert Mugabe atatia saini ili iwe sheria. Chama cha rais Mugabe cha ZANU-PF kimewalaumu wabunge wa MDC kwa kujaribu kuchelewesha kuidhinishwa rasimu hiyo ya katiba ili uchaguzi mkuu pia uchelewe kufanyika. Katiba mpya ni miongoni mwa masharti muhimu yaliyotolewa na jamii ya kimataifa kwa ajili ya kufanyika uchaguzi huru nchini Zimbabwe.

0 comments:

Post a Comment