Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 9 May 2013

Mawaziri waliopendekezwa Kenya waanza kusailiwa



Kamati ya bunge la Kenya inayohusika na kuwachunguza watu wanaoteuliwa kushika nyadhifa serikalini imeanza kazi ya kuwasaili mawaziri 16 waliopendekezwa na Rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake William Ruto majuma mawili yaliyopita. Leo alhamisi, kamati hiyo imewasaili mawaziri 5 kati ya 16 na zoezi hilo linatarajiwa kuendelea hadi Jumamosi. Kamati hiyo inayoongozwa na spika wa bunge, Justin Muturi imefanya usaili huo mbele ya vyombo vya habari katika ukumbi wa mikutano ya kimataifa wa KICC. Miongoni mwa waliosailiwa ni pamoja na Bi. Amina Mohammed ambaye amependekezwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bw. Henry Roticha (Fedha), Anne Waiguru (Ugatuzi), Raychelle Omamo (Ulinzi) na Jacob Kaimenyi (Elimu, Sayansi na Teknolojia). Iwapo mawaziri hao 16 wataidhinishwa na kamati hiyo ya bunge, majina yao yatawasilishwa bungeni ili wabunge wote wawapigie kura.

0 comments:

Post a Comment