Chama cha Wananchi (CUF) kimesema kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015, kimejipanga kuhakikisha kinafanya kampeni kuhamasisha wananchi wanajiunga nacho kuanzia ngazi ya kijiji.
Akizungumza baada ya kikao cha kutathmini
mafanikio ya mradi wa maendeleo, Mjumbe wa Baraza Kuu la Uongozi Taifa,
Mbarala Maharagande alisema chama hicho kinajipanga kwa uchaguzi mkuu
ujao.
Maharagande alisema CUF haitaki kurejea tena
makosa ya kupoteza majimbo ambayo yalionyesha kuwa chini ya chama hicho,
hivyo kitaanzisha mafunzo kwa viongozi wake wakiwamo madiwani na
wenyeviti wa serikali za mitaa.
Alisema mbinu hiyo inaratibiwa na uongozi wa juu
wa taifa wa chama hicho, kila kiongozi mwenye dhamana anatakiwa
kuhakikisha eneo lake linakuwa chini ya CUF.
“CUF kinavyoungwa mkono na Watanzania hivi sasa
tunajipanga kweli hakuna kulala tena, uchaguzi mkuu upo mbele yetu
wenzetu wakae chonjo,” alisema Maharagande.
Kuhusu mafanikio ya mradi wa maendeleo wa chama
hicho unaofadhiliwa na Redicale, Maharagande alisema wameibua kero
nyingi na kujionea migogoro ya kupandikizwa.
Alisema Serikali ndiyo inayokaribisha umaskini
wakati nchi imejaa utajiri, hivyo kuwashauri wananchi kubadilisha
mwelekeo kwa kuchagua CUF.
Alisema nchi ina rasilimali nyingi ya gesi, mafuta
na madini kitu ambacho kinatosha Serikali kutekeleza miradi yake bila
kutegemea wafadhili.
Akizungumza katika kikao hicho, Mratibu wa Mradi
wa CUF/RV Mkoa wa Tanga, Mussa Mbarouk, alitaka Serikali kutekeleza
ahadi zake ilizotoa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliopita.
0 comments:
Post a Comment