Waziri Mkuu wa Libya ameziomba nchi za Kiafrika zitoe mashirikiano kwa
nchi hiyo ili kuwezesha kurejeshwa fedha za Libya zilizoibiwa. Ali
Zaidan Waziri Mkuu wa Libya ameziomba nchi za Kiafrika kushirikiana ili
kufanikisha kurejeshwa fedha za Libya zilizoibiwa na kuwakabidhi watu
wa karibu wa Kanali Muammar Gaddafi kiongozi wa zamani wa Libya
aliyeng'olewa madarakani wanaosakwa na serikali. Waziri Mkuu wa Libya
pia amesema vitega uchumi vya nchi hiyo vilivyoko katika nchi za
Kiafrika ni miongoni mwa mali za raia wa Libya na kuzitaka nchi za
Kiafrika kuzilinda mali hizo.
0 comments:
Post a Comment