Watu wasiopungua saba jana waliuawa huko Bangui mji mkuu wa Jamhuri ya
Afrika ya Kati katika mapigano makali kati ya vikosi vilivyotwaa
madaraka mwezi uliopita na wanamgambo vijana watiifu kwa rais
waliyempindua madarakani nchini humo. Jenerali Moussa Dhaffane ambaye
amesema amekuwa akikaimu nafasi ya msemaji wa serikali ameeleza kuwa
mapigano ya jana yalianza baada ya vikosi viliyotwaa madarakani huko
Jamhuri ya Afrika ya Kati kupiga doria katika ngome ya wapiganaji
watiifu kwa Francois Bozize ambao walipatiwa silaha wakati waasi wa
Seleka waliposonga mbele kuelekea mji mkuu Bangui. Mkuu wa Hospitali ya
Bangui amesema kuwa watu saba waliuawa katika mapigano ya jana na kwamba
idadi ya majeruhi inaongezeka kwa kuwa majeruhi wengine wanaendelea
kufikishwa hospitalini kwa ajili ya matibabu.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment