Tume ya Uchaguzi ya Venezuela imemtangaza Nicolas Maduro kuwa
mshindi wa uchaguzi wa rais uliofanyika jana nchini humo. Maduro amepata
asilimia 50.66 ya kura huku mpinzani wake Henrique Capriles akipata
asilimia 49.06. Capriles amepinga matokeo hayo ya uchaguzi. Tume ya
Uchaguzi ya Venezula leo imeripoti kuwa zaidi ya asilimia 99 ya kura
zimehesabiwa hadi sasa na kwamba matokeo ya uchaguzi hayawezi
kubadilika. Nicolas Maduro amesema amepata ushindi halali na wa
kikatiba.
Maduro ameahidi katika uongozi wake kuendeleza sera za kisoshalisti za kiongozi aliyemtangulia marehemu Hugo Chavez.
Maduro ameahidi katika uongozi wake kuendeleza sera za kisoshalisti za kiongozi aliyemtangulia marehemu Hugo Chavez.
0 comments:
Post a Comment