Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Wednesday 24 April 2013

Wizara yashtushwa baa zinazojengwa maeneo ya shule



Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imeziagiza bodi na kamati za shule nchini kupitia upya mikataba iliyoingiwa kati ya shule na wafanyabiashara waliojenga maduka, baa zikamo nyumba za kulala wageni kwenye uzio wa shule.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Elimu, Kassim Majaliwa, alitoa agizo hilo jana wakati akizungumza katika kipindi cha Kumepambazuka kinachorushwa na Radio One Sterio.

Majaliwa alisema kuruhusu ujenzi wa baa, maduka na nyumba za kulala wageni kwenye uzio wa shule kunaleta athari kwa wanafunzi kimasomo, hivyo kamati za shule na bodi ziangalie upya mikataba hiyo ikiwezekana isitishwe.

Alisema serikali imeshatoa waraka kwa wakurugenzi wa halmashauri kusimamia suala hilo na kwamba mkurugenzi atakayeshindwa kufanya hivyo atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

“Tumeshatoa waraka kwa wakurugenzi wasimamie suala la upitiaji wa mikataba hiyo na kwa mkurugenzi atakayeshindwa kufanya hivyo itabidi tumchukulie hatua kama atakuwa ameshindwa kuwajibisha viongozi wa shule husika,” alisema Majaliwa.

Kwa muda mrefu kumekuwa na tatizo la baadhi ya viongozi wa shule kwa kushirikiana na bodi na kamati za shule kuingia mikataba na wafanyabiashara  ambao wanajenga maduka na baa katika uzio wa shule kwa lengo la kujipatia fedha bila kujali athari wanazoweza kupata wanafunzi.

0 comments:

Post a Comment