Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 11 April 2013

WB:Uharamia Somalia waathiri biashara ya kimataifa

Benki ya Dunia imesema kwenye ripoti yake mpya kuwa, uharamia wa baharini nchini Somalia umesababisha kuongezeka gharama ya kuendesha biashara ya kimataifa kwa zaidi ya dola bilioni 18 kila mwaka. Ripoti hiyo aidha imesisitiza kuwa mfumuko wa bei za bidhaa muhimu pia umesababishwa kwa kiwango fulani na tatizo la uharamia wa baharini katika pwani ya Somalia. Hata hivyo, Benki ya Dunia imekiri kwamba uharamia umepungua mno katika kipindi cha miaka 2 iliyopita. Imesema mafanikio hayo yametokana na juhudi za nchi mbalimbali kupeleka wanajeshi wa majini kupiga doria katika maji ya kimataifa karibu na pwani za Somalia na Aden. Mwaka 2009 zaidi ya meli 100 zilitekwa nyara na maharamia huko Somalia jambo lililotoa pigo kubwa kwa biashara ya mafuta na matunda katika soko la kimataifa.

0 comments:

Post a Comment