Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 11 April 2013

Boko Haram yakataa msamaha wa serikali Nigeria

 
Kiongozi wa kundi la waasi la Boko Haram nchini Nigeria, Abubakar Shekau amesema kundi hilo halihitaji msamaha wa serikali na kwamba litaendeleza mapambano dhdi ya kile alichokiita uchafu wa Wamagharibi. Shekau amesema serikali ndiyo inayopaswa kuliomba msamaha kundi hilo. Pia ametoa orodha ndefu ya jinai anazodai serikali imewatendea Waislamu wa Nigeria. Hii ni katika hali ambayo, serikali ya Nigeria imetangaza kuwa iko tayari kutoa msamaha kwa wanachama wa Boko Haram ambao wako tayari kusitisha mashambulizi yao dhidi ya maafisa wa usalama pamoja na raia nchini humo. Mpango huo wa msamaha umeratibiwa na viongozi wa Kiislamu kutoka maeneo ya kaskazini mwa Nigeria ambao wamedai kwamba wahanga wakubwa wa hujuma za Boko Haram ni Waislamu wenyewe. Hata hivyo wanasiasa wa kusini mwa nchi wameijia juu serikali wakiitaka kutumia mkono wa chuma kukabiliana na kundi hilo ambalo limetangaza hadharani mfungamano wake na mtandao wa kigaidi wa Al-Qaeda.  

0 comments:

Post a Comment