Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 25 April 2013

"Washington ilipanga mashambulizi ya Boston"

                     
Mbunge wa chama cha upinzani cha Republicans nchini Marekani amedai kwamba serikali ya nchi hiyo ndiyo iliyopanga mashambulizi ya mabomu huko Boston wakati wa mashindano ya mbio za masafa marefu maarufu kama Boston Marathon. Stella Tremblay, amesema taarifa ya serikali kuhusu jinsi mashambulizi hayo yalivyotokea haina muwala wala mtiririko na kwa mantiki hiyo inaweza kutiliwa shaka. Amesema kuna ushahidi unaoonyesha kuwa mabomu hayo yalitegwa na serikali ili kufikia malengo yake haramu. Hata hivyo, mbunge huyo wa New Hampshire hakufafanua kuhusu ushahidi huo. Amesema Marekani imekuwa ikitumia ndege zisizo na rubani kuwaua watu wasio na hatia na kana kwamba haijatosheka, sasa imeamua kumwaga damu za Wamarekani ndani ya nchi yao. Serikali ya Washington haijasema lolote kuhusu tuhuma hizo.

0 comments:

Post a Comment