Wananchi wa Kordofan kaskazini nchini Sudan, wamefanya maandamano ya
kupinga mashambulizi ya waasi jimboni hapo. Maandamano hayo yalifanyika
hapo jana Jumapili katika eneo la Umm Ruwaba wakipinga mashambulizi
yanayofanywa na waasi waHarakati ya Ukombozi ya Wananchi wa Sudan (SPLA)
tawi la kaskazini mwa Sudan. Waandamanaji pia walitoa nara wakiitaka
serikali ya Khartoum kuchukua hatua kali dhidi ya waasi nchini humo.
Siku ya Jumamosi Msemaji wa jeshi la Sudan al- Sawarmi Khalid aliwambia
waandishi wa habari kuwa, jeshi la Sudan lilikuwa limeanzisha msako
mkali katika eneo hilo la Umm Ruwaba baada ya kuwafurusha waasi wa(SPLA)
tawi la kaskazini waliokuwa wamevamia eneo hilo. Mashambulizi ya waasi
hao yalijiri saa chache baada ya kutangazwa kuvunjika mazungumzo ya
serikali ya Khartoum na ujumbe wa harakati hiyo yaliyokuwa yakifanyika
mjini Addis Ababa, Ethiopia, chini ya usimamizi wa Thabo Mbeki
mpatanishi wa Umoja wa Afrika katika mazungumzo ya amani ya Sudan.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment