Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Monday 29 April 2013

Wizara nchini Libya yanasurika kushambuliwa



Waziri Mkuu wa Libya Ali Zeidan ametangaza kuwa, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Libya imenusurika kushambuliwa na watu wenye silaha. Zeidan amesema hayo katika kikao na waandishi wa habari na kuongeza kuwa, watu wenye silaha waliivamia wizara hiyo kwa lengo la kuishambulia lakini polisi walifanikiwa kuzima haraka jaribio hilo la shambulizi. Aidha waziri mkuu huyo wa Libya ameongeza kuwa, watu wenye silaha pia walikuwa wamepanga kutekeleza shambulizi jingine dhidi ya jengo la idara ya habari ya Libya na kwamba, shambulizi hilo limezimwa kwa juhudi za polisi wa nchi hiyo. Ali Zeidan amesisitiza kuwa, serikali ya Libya iko makini dhidi ya mashambulizi kama hayo na kwamba, haitorudi nyuma katika mapambano yake dhidi ya wahalifu na watu wanaotaka kuhatarisha usalama wa nchi hiyo. Kabla ya hapo siku ya Jumapili pia ilikuwa imetangazwa kuwa, kundi la watu wenye silaha lilikuwa lilizingira jengo la Wizara ya Mashauri ya Nje ya nchi hiyo. Viongozi wa serikali ya sasa ya Libya wametakiwa kuzima  harakati za wafuasi wa utawala uliong'olewa madarakani nchini humo ili kuepusha matukio kama hayo.

0 comments:

Post a Comment