Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya an-Nahdha ya Tunisia, Dakta Rashid
al Ghanushi amesisitizia juu ya kufungamana harakati hiyo na mfumo wa
uwiano wa bunge nchini humo. Al Ghanushi amesisitiza kuwa, harakati ya
an-Nahdha inasisitiza juu ya kuwepo mfumo wa uwiano wa bunge ambao kwa
mujibu wake kutakuwepo makubaliano juu ya mamlaka na majukumu ya rais
na waziri mkuu wa nchi. Aidha amesisitiza kuwa, lengo la an-Nahdha
katika kuimarisha mfumo huo wa bunge ni kwa ajili ya kukabiliana na
mfumo wa udikteta. Hivi karibuni viongozi wa vyama vya siasa vinavyounda
serikali ya Tunisia, walijadiliana kuhusiana na mfumo wa kisiasa wa
hapo baadaye wa nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika na wadhifa wa rais na
waziri mkuu wa nchi. Hata hivyo mazungumzo hayo hayajakuwa na natija
mpaka sasa.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment