Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Tuesday 30 April 2013

Sudan yawasamehe waliokula njama za mapinduzi

21Jumaadal Aakhir,1434 Hijiriyah/ May 01,2013 Miyladiyah
Rais Omar Hassan al Bashir wa Sudan ametoa msamaha kwa askari ambao hivi karibuni walikula njama za kufanya mapinduzi dhidi ya serikali ya nchi hiyo. Rais al Bashir ametoa msamaha kwa askari saba wa idara ya usalama na ulinzi wa taifa ya Sudan ambao walitiwa mbaroni baada ya kutuhumiwa kula njama za kutaka kuiangusha serikali iliyoko madarakani nchini humo. Kwa mujibu wa habari hiyo, msahama huo umetolewa baada ya askari hao kuomba radhi kwa Rais al Bashir hivi karibuni. Itakumbukwa kuwa wiki kadhaa zilizopita Rais Omar Hassan al Bashir wa Sudan alitoa msamaha kwa kiongozi mmoja nchini humo aliyetiwa mbaroni kwa tuhuma za kupanga njama kama hizo sambamba na kuwahukumu kifungo cha miaka miwili hadi minane watuhumiwa wengine sita wa kesi hiyo. Weledi wa masuala ya kisiasa waliutaja msamaha huo kuwa mwanzo wa kuelekea kwenye maelewano ya kisiasa nchini Sudan.

0 comments:

Post a Comment