Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Tuesday 30 April 2013

Misri yajiondoa katika mazungumzo ya nyuklia

Misri imejiondoa katika mazungumzo ya Mkataba wa Kuzuia Uzalishaji na Usambazaji wa Silaha za Nyuklia (NPT) unaoendelea huko Geneva Uswisi ukilalamikia kushindwa jamii ya kimataifa kutekeleza azimio la kulifanya eneo la Mashariki ya Kati lisiwe na silaha hata moja ya nyuklia. Leo Jumatatu Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri imetoa taarifa na kueleza kuwa Cairo imeamua kuacha kushiriki katika mazungumzo hayo ya wiki mbili kufuatia kushindwa nchi nyingine kutekeleza azimio la mwaka 1995 linalotaka kuhakikisha kuwa eneo la Mashariki ya Kati halina silaha za nyuklia.  Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri imeeleza kuwa Cairo haiwezi kusubiri milele utekelazaji wa uamuzi huo. Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri imesema kuwa hatua ya nchi hiyo ya kusitisha kushiriki kwenye mkutano wa Geneva ni sawa na kutuma ujumbe mzito kwamba Cairo haikubaliani na  hatua ya jamii ya kimataifa ya kutolipa uzito suala la kuangamizwa silaha za nyuklia katika eneo la Mashariki ya Kati. Itakumbukwa kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel ndilo dola pekee linalomiliki silaha za nyuklia katika eneo la Mashariki ya Kati na hadi leo unakaidi mashinikizo ya jamii ya kimataifa ya kuruhusu wakaguzi wa nyuklia kutembelea vinu vyake vya nyuklia.

0 comments:

Post a Comment