Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Tuesday 30 April 2013

Rais wa zamani wa Tunisia apata kifungo cha maisha



Kwa mara nyingine mahakama ya kijeshi nchini Tunisia imemuhukumu dikteta wa nchi hiyo aliyekimbia nchi kifungo cha maisha jela bila ya kuwepo mahakamani. Hii ni mara ya tatu kwa mahakama hiyo ya kijeshi nchini Tunisia kumuhukumu dikteta Zainul Abidin Bin Ali kwa makosa ya mauaji dhidi ya wananchi katika harakati za mapinduzi ya wananchi za mwaka 2010 na 2011. Wakati huo huo Rafik Haj Kassem, Waziri wa Mambo ya Ndani wa utawala wa Bin Ali, amehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela huku Ali Saryati, Mkuu wa zamani wa Idara ya Usalama ya Tunisia akifutiwa tuhuma zote zilizokuwa inamkabili. Inasemekana kwamba, familia ambayo ilimpoteza mtu mmoja au kujeruhiwa watu wawili wa familia hiyo katika harakati za mapinduzi hayo, italipwa kuanzia Dinar elfu 12 hadi laki moja sarafu ya Tunisia, sawa na Dola za Kimarekani elfu nane hadi elfu sabini.

0 comments:

Post a Comment