27Jumaadal ula,1434 Hijiriyah/ April 08,2013 Miyladiyah
Watu 18 wameuawa nchini Afghanistan wakiwemo watoto wadogo 11 kufuatia
mashambulio ya anga ya vikosi vya Jumuiya ya kijeshi ya NATO mashariki
mwa Afghanistan. Wasifullah Wasifi, Msemaji wa Jimbo la Kunar amesema
kuwa, mashambulio hayo ya anga ya NATO yamefanywa katika kijiji cha
Shighal katika viunga vya jimbo hilo na kwamba, yamefanyika baada ya
vikosi hivyo vya NATO na vile vya serikali ya Afghanistan kukabiliwa na
mashambulio ya Taliban. Taarifa zaidi kutoka nchini Afghanistan zinasema
kuwa, mbali na watoto wadogo, miongoni mwa waliouawa katika mashambulio
hayo ya anga ya Jumuiya ya Kijeshi ya NATO wamo wanawake sita. Rais
Hamid Karzai wa Afghanistan amelaani vikali mashambulio hayo na ametoa
amri ya kufanyika uchunguzi mara moja kuhusiana na mashambulio hayo.
Taarifa ya Ikulu ya Rais wa Afghanistan imesisitiza kwamba, serikali
yake inalaani operesheni yoyote ile ya kijeshi inayopelekea kuuawa raia
wasio na hati yoyote. Mauaji hayo yanakuja siku moja tu baada ya
Wamarekani watano kuuawa akiwemo mwanadiplomasia mmoja kijana kufuatia
mashambulio mawili tofauti ya Taliban mashariki na kusini mwa nchi hiyo
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment