27Jumaadal ula,1434 Hijiriyah/ April 08,2013 Miyladiyah
Wawakilishi wa nchi wahisani na mashirika ya utoaji misaada wanaendelea
kukutana katika mji mkuu wa Qatar, Doha, kwa shabaha ya kuunga mkono
mkakati wa kuchangisha mabilioni ya dola kwa ajili ya kulijenga upya
jimbo la Darfur la Sudan baada ya mzozo wa muongo mmoja. Kiongozi wa
ujumbe wa Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Jorg
Kuhnel amesema mkutano huo ni fursa ya kipekee kwa Sudan na kubadilisha
hatma ya jimbo hilo lililokumbwa na hali ya mchafukoge. Taarifa kutoka
Doha Qatar zinasema kuwa, mkutano huo wa siku mbili unahudhuriwa na
wajumbe 400 kutoka maeneo mbalimbali na unafanyika kwa mujibu wa mkataba
wa amani wa Julai mwaka 2011, ambapo Sudan ilitiliana saini na
muungano wa makundi ya waasi mjini Doha. Duru za karibu na mkutano huo
zinasema kuwa, mkutano huo unakusudia kukusanya Euro bilioni 5.5 ili
kuutekeleza mpango wa miaka sita wa kulisaidia jimbo la Darfur.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment