Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Sunday 7 April 2013

Azawad yasisitiza kujitawala kaskazini mwa Mali


                                    27Jumaadal ula,1434 Hijiriyah/ April 08,2013 Miyladiyah
 Harakati ya Ukombozi ya Azawad imetangaza kuwa, ingali inasisitiza juu ya mamlaka ya kujitawala eneo la kaskazini mwa Mali. Viongozi wa Harakati ya Azawad wamesisitiza juu ya kuweko mazungumzo yenye lengo la kupatikana amani na kuhitimishwa makumi ya miaka ya kukaliwa kwa mabavu eneo hilo na serikali kuu ya Mali.
 Msimamo huo wa Harakati ya Ukombozi wa Azawad ni jibu kwa ombi la Laurent Fabius Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Ufaransa aliyeitaka harakati hiyo iweke chini silaha na iingie katika mchakato wa kisiasa nchini Mali.

Wakati huo huo, imeelezwa kuwa, hali ya kibinaadamu nchini Mali inazidi kuwa mbaya. Ripoti zinasema kuwa, watoto ndio wahanga wakuu wa mapigano na vita vya Mali.

Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetangaza kuwa, watoto wanaokaribia laki mbili wanakabiliwa na hatari ya kufariki dunia au kujeruhiwa na milipuko ya mabomu nchini humo. UNICEF imesema kuwa mabomu hayo ambayo bado hayajalipuka yamesalia nchini Mali tangu mwanzoni mwa mapigano yanayoendelea sasa kati ya vikosi vya majeshi ya Ufaransa na makundi yenye silaha katike eneo la kaskazini mwa Mali.

0 comments:

Post a Comment