27Jumaadal ula,1434 Hijiriyah/ April 08,2013 Miyladiyah
Rais mstaafu wa awamu ya tatu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania amewaasa Watanzania na vitendo vitakavyopelekea kuvurugika
amani ya nchi hiyo ya Afrika Mashariki. Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa
amesifia utawala wake kwa kuongoza taifa bila ya kubaguana na
amesikitishwa na matukio ya udini, ambayo yanaashiria kuvuruga amani na
utulivu wa Tanzania katika siku za karibuni.
Mkapa amesema kuwa, taifa
la Tanzania linapaswa kujenga utamaduni wa kupendana, huku akilaumu kuwa
kizazi kipya cha uongozi kimeanzisha mambo ya ajabu ya kukosa upendo na
kudhalilishana.
Onyo la Mkapa limekuja siku chache baada ya Rais Jakaya
Kikwete kukemea mambo ya kidini na kutetea serikali yake kwamba
haiongozi kwa misingi ya ubaguzi.
Matamshi ya Rais Kikwete na mtangulizi
wake Mkapa yametolewa katika kipindi hiki ambapo Tanzania imetikiswa na
matukio yenye mwelekeo wa chuki za kidini.
Matukio makubwa yakiwa yale
ya kuuawa Padri Evarist Mushi huko Zanzibar na Mchungaji Mathayo Kachila
wa Geita. Pia kupigwa risasi kwa Padre Ambrose Mkenda na kumwagiwa
tindikali kwa Sheikh Fadhil Soraga na vurugu za mambo ya kuchinja katika
mikoa ya Geita na Mbeya.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment