Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Monday, 1 April 2013

Mkapa: Watanzania! tusitangulize udini kwenye Katiba

Rais mstaafu wa awamu ya tatu nchini Tanzania Bwana Benjamin  Mkapaamewataka Watanzania kutotoa maoni kuhusiana na Katiba mpya kwa misingi ya udini. Mkapa ameyasema hayo mjini Masasi ambapo ameliasa taifa la Tanzania kujiepusha na utoaji maoni ya Katiba mpya kwa misingi ya dini. Mkapa amesema Katiba ijayo haipaswi kuwa na itikadi za kidini kwa kuwa zinaweza kuliangamiza taifa. Rais huyo mstaafu wa Tanzania amesema kama ninavyomnukuu “Wapo watakaopata uwakilishi kupitia rasimu ya Katiba ya nchi. Namwomba Mwenyezi Mungu awape mwanga, muhakikishe jambo moja tu ambalo litakuwa msingi mkubwa wa amani na maendeleo na umoja wa taifa letu. Watupatie Katiba ambayo inatoa fursa kamilifu ya kila mtu kuwa na imani yake.“ Mwisho wa kunukuu.  Vilevile rais huyo mstaafu wa Tanzania amesisitizia juu ya nchi hiyo kuepukana na imani moja rasmi kama ambavyo nchi hiyo haina kabila moja.

0 comments:

Post a Comment